Saturday, 30 June 2012
MWANACHAMA MPYA
Tunamkaribisha mwanachama mpya kwa jina Dida Haji, tumemkubali Bi. Dida kwa kipengele kipya cha chama "Viongozi wa chama wanao uwezo wa kumkubali ama kumkataa mtu yoyote anayetaka kujiunga na chama" Bi Dida Haji karibu Shadhily
Friday, 29 June 2012
ADA YA CHAMA NA MADENI
Asalaam Aleykum, wanachama wote tunasisitiza kwa yeyote ataeweka pesa kwenye account aweke reference jina lake ili tuweze kujuwa ni nani ameweka hizo pesa. Na kwa wote wanaodaiwa ada ya mwaka jana, naomba wamalizie deni, mnaturudisha nyuma. Shukrani, Mweka hazina, Fathiya Said
Thursday, 28 June 2012
ADA YA CHAMA
Je mwanachama apewe muda gani alipe Ada ya chama? Na sheria ipi ichukuliwe asipolipa Ada baada ya miezi 6. Naomba wanachama wachangie maoni yao
Wednesday, 27 June 2012
ADDRESS YA KURUDISHA FOMU
Kwa wanachama waliojaza fomu na wanataka kuzirudisha, Address yangu, 5 Waldstock house, 47 Carronade place, Thamesmead, SE28 0EE
Tuesday, 26 June 2012
MWANACHAMA MPYA
Mwanachama mpya anataka kujiunga na Shadhily jina lake Dida Haji anakaa Reading. Hivyo viongozi mnatakiwa kutoa maoni yenu kama mmemkubali ama mmemkataa.
NIDHAMU
Wanachama wote tunawakumbusha kwamba tunataka kutengeneza kipengele cha NIDHAMU katika katiba yetu, ili kiweze kuwa na MAAMUZI YAKE. Tunawakumbusha nyote kutoa mawazo yenu kwa pamoja, Mwenyekiti Msaidizi (Ibrahimu Salim)
SHUKRANI
ASALAM ALEYKUM Ndungu zangu.Mimi na family yangu tunatanguliza shukurani zetu zadhati kutupa nafasi ya kuwakaribisha kuwa pamoja. Na tunaomba radhi kama kulikuwa na upungufu wowote uliojitokeza. Ahsanteni sana, Bw. Zubery na family yake
Saturday, 23 June 2012
MKUTANO
Ahsanteni sana wanachama wote mliojitokeza kuja kwenye mkutano, kwa niaba ya Shadhily tunawashukuru Zubbery Qambertato'g na Mwanaana Zubbery Aboubakary kwa kutualika na kutukarimu. Mkutano ujao utafanyika Slough, tarehe 29 September 2012. Ahsante Fatouma Abdulsamad kwa kutualika. Vilevile tunawakaribishe wanachama watatu wapya, Fatma Abdulsamad, Mariamu Manding'o na Swada Karanda. Karibuni Shadhily, Katibu
Wednesday, 20 June 2012
MADA YA KIKAO TAREHE 23 JUNI
Mada ya kikao tarehe 23 juni
1. Ada ya chama. Kwa wale amabao hawajatimiza malipo. 30 minutes
2.utaratibu wa kusajili wanachama wapya. (katiba). 15 min.
3. Mchango wa misiba wa ndugu (katiba). 15 minus
4. Account number na Standing Order. 15 min.
1. Ada ya chama. Kwa wale amabao hawajatimiza malipo. 30 minutes
2.utaratibu wa kusajili wanachama wapya. (katiba). 15 min.
3. Mchango wa misiba wa ndugu (katiba). 15 minus
4. Account number na Standing Order. 15 min.
Subscribe to:
Posts (Atom)