Tuesday, 2 October 2012
SHUKRANI
Kwa niaba ya Shadhily Society naomba kutoa Shukrani za dhati kwa Hannat na Yusuph Family kwa kuwezesha kufanyika kikao chetu, kama kuna jambo tumewakosea tunaomba mtusamehe.. Ahsanteni
Saturday, 22 September 2012
MAJINA YA KHITMA
Asalaam Aleykum, naomba kila mwanachama aandike majina kwaajili ya kusoma Khitma. Ahsanteni
ADDRESS YA KIKAO
Asalaam Aleykum, kikao chetu kitafanyika tarehe 29/09/12, saa nane mchana, address 79 Roxwell road, Barking, Essex, IG11 0PS. Ahsanteni
MCHANGO WA CHAKULA
Asalaam Aleykum, nimeshatuma Account number kwaajili ya chakula kwa kila mwanachama, kwa wale wasiopata nijulisheni, naomba kila mwanachama achangie £15 Family na £10 single. Kuhusu Ada ya chama naomba kila mwanachama awe amemaliza Ada kabla ya kufika kwenye mkutano. Kuhusu Mada ya mkutano tutazungumzia kuhusu jinsi gani tutafanya kwa wale wanachama watakaoshindwa kutoa Ada, na kama mwanachama yoyote anayo MADA aseme ili tuweze kuijadili siku ya kikao. Ahsanteni
MADA YA KWENYE KIKAO
Asalaam Aleykum, Naomba wanachama wote mchangie MADA ambayo mnataka izungumzwe kwenye mkutano na pia kuhusu marekebisho ya KATIBA manataka kipengele gani kiangaliwe ama kibadilishe. naomba maoni yenu kabla ya mkutano. Ahsanteni
Saturday, 21 July 2012
DUA - MILTON KEYNES
Tutakuwa na mawaidha jumamosi tarehe 28 halafu tutakuftari sote hapa Milton Keynes, karibuni sana waislam wote, Yanaanza saa 10 jioni ni ndugu zetu wale wa London Arbil wa Taquwa wale ambao walikuwepo kwangu na dufu kama mnawakumbuka. Mwenyekiti Msaidizi, Ibrahim Salim
RAMADHAAN MUBARAK
Asalaam Aleykum, nawatakieni Ramadhaan Kareem ndugu zangu, naomba Mola awawezeshe mfunge Ramadhaaan kwa salama, naomba Mola awawezeshe muimalize Ramadhaan kwa salama, naomba Mola wakubalieni dua zenu na naomba Mola awasemehini makosa yenu, Ameen
Saturday, 30 June 2012
MWANACHAMA MPYA
Tunamkaribisha mwanachama mpya kwa jina Dida Haji, tumemkubali Bi. Dida kwa kipengele kipya cha chama "Viongozi wa chama wanao uwezo wa kumkubali ama kumkataa mtu yoyote anayetaka kujiunga na chama" Bi Dida Haji karibu Shadhily
Friday, 29 June 2012
ADA YA CHAMA NA MADENI
Asalaam Aleykum, wanachama wote tunasisitiza kwa yeyote ataeweka pesa kwenye account aweke reference jina lake ili tuweze kujuwa ni nani ameweka hizo pesa. Na kwa wote wanaodaiwa ada ya mwaka jana, naomba wamalizie deni, mnaturudisha nyuma. Shukrani, Mweka hazina, Fathiya Said
Thursday, 28 June 2012
ADA YA CHAMA
Je mwanachama apewe muda gani alipe Ada ya chama? Na sheria ipi ichukuliwe asipolipa Ada baada ya miezi 6. Naomba wanachama wachangie maoni yao
Wednesday, 27 June 2012
ADDRESS YA KURUDISHA FOMU
Kwa wanachama waliojaza fomu na wanataka kuzirudisha, Address yangu, 5 Waldstock house, 47 Carronade place, Thamesmead, SE28 0EE
Tuesday, 26 June 2012
MWANACHAMA MPYA
Mwanachama mpya anataka kujiunga na Shadhily jina lake Dida Haji anakaa Reading. Hivyo viongozi mnatakiwa kutoa maoni yenu kama mmemkubali ama mmemkataa.
NIDHAMU
Wanachama wote tunawakumbusha kwamba tunataka kutengeneza kipengele cha NIDHAMU katika katiba yetu, ili kiweze kuwa na MAAMUZI YAKE. Tunawakumbusha nyote kutoa mawazo yenu kwa pamoja, Mwenyekiti Msaidizi (Ibrahimu Salim)
SHUKRANI
ASALAM ALEYKUM Ndungu zangu.Mimi na family yangu tunatanguliza shukurani zetu zadhati kutupa nafasi ya kuwakaribisha kuwa pamoja. Na tunaomba radhi kama kulikuwa na upungufu wowote uliojitokeza. Ahsanteni sana, Bw. Zubery na family yake
Saturday, 23 June 2012
MKUTANO
Ahsanteni sana wanachama wote mliojitokeza kuja kwenye mkutano, kwa niaba ya Shadhily tunawashukuru Zubbery Qambertato'g na Mwanaana Zubbery Aboubakary kwa kutualika na kutukarimu. Mkutano ujao utafanyika Slough, tarehe 29 September 2012. Ahsante Fatouma Abdulsamad kwa kutualika. Vilevile tunawakaribishe wanachama watatu wapya, Fatma Abdulsamad, Mariamu Manding'o na Swada Karanda. Karibuni Shadhily, Katibu
Wednesday, 20 June 2012
MADA YA KIKAO TAREHE 23 JUNI
Mada ya kikao tarehe 23 juni
1. Ada ya chama. Kwa wale amabao hawajatimiza malipo. 30 minutes
2.utaratibu wa kusajili wanachama wapya. (katiba). 15 min.
3. Mchango wa misiba wa ndugu (katiba). 15 minus
4. Account number na Standing Order. 15 min.
1. Ada ya chama. Kwa wale amabao hawajatimiza malipo. 30 minutes
2.utaratibu wa kusajili wanachama wapya. (katiba). 15 min.
3. Mchango wa misiba wa ndugu (katiba). 15 minus
4. Account number na Standing Order. 15 min.
Monday, 28 May 2012
HURUMA YA KUKU KWA VIRANGA VYAKE
Asalam alykum, baada ya salaam nina mshukuru Allahsubhanahu wataala na rehma na amani zimuendendee kipenzi chake taalaa saYyidna muhammadin na family yake na maswahaba pia ni kawaida kumuona kuku akimuitiya kifaranga chakula wakati yeye mwenyewe ana njaa au akiwafunika viranga wake wasipate jua ilhali yeye anaunguwa na jua halikadhalika na mvua anafanya hivyo hivyo ili vifaranga visilowe na mara ngapi huyo kuku pia anajitiya hatarini ili vifaranga viwe salama?huruma iliyoje ushujaa ulioje. Lakini baada ya yote haya kifaranga kikikuwa hakina tena habari na mama mzazi yule na wala sijuwi kama kiliwahi kumuuliza mama ulinileaje? Alhamdu lillahi sisi wanaadaamu hukumbuka haya kuwa mama zetu waliyoyafanya haya yote na kupita haya walivumila kilio chetu cha usiku kucha walitusafisha tulipokuwa tukijichafua na nepi au kipande cha kanga. Kuku yeye hakubahatika kuchenji nepi na si pempazi. Hakika Allah hakumpendelea mama aliposema nani anafaa kumpenda zaidi mama yako na mama yako halafu baba yako Allah anatufundisha aliposema waqadhwaa rabbuka allaa. Taabudu illa iyyaahu wabilwalidaini i7saana imma yablughanna 3in-daka lkibaru a7huduma au kila huma falaa taqul lahuma uffin walaa tanharhumaa waqul lahumaa qaulan kariima wakhfidhlahuma jana7a dhulli min ra7matin waqul lahumaa qaulan kariima maana yake ni amehukumu ameamrisha ya kuwa asiabudiwe yeyote isipokuwa yeye tu Allah jalla jaluhu na kuwatendeya wema wazazi wako wawili wakifikiya uzee mmojawapo au wote wawili usiwaambiye nyamaza au usiwakaripie na uwaambie maneno mazuri, na uwashushie ubawa wa upole kama afanyavyo kuku na useme allh nakuomba uwasamehe na uwashushie rehma kama walivyonileya mimi wakati niko mdogo. Hassan Nurdin
Sunday, 27 May 2012
TUMSHUKURU ALLAH (ALHAMDULLILLAH)
Asalam alykum, Ukitaka kushukuru muangalie aliyechini yako halafu utaona Allah amekupenda kiasi gani, miguu miwili Alhamdulillah. Kuna wengine hawana macho, masikio, afya na hata chakula. Na vingine vingi ambavyo hatuwezi kuvifikiria. Allah ametuhakikishia ukishukuru (Allah) atakuzidishia. Alhamdulillahi. Hassan Nurdin
Friday, 25 May 2012
MCHANGO WA KUMFARIJI MFIWA
Asalaam Aleykum, Kuhusu mchango wa marehemu bibi yake Aziza Said. Tunaomba wanachama wote wajitolee kumchangia mfiwa ili aweze kupeleka chochote nyumbani ama kufanya hitma. Kama mnavyojua mfuko wetu hauwezi kumsaidia ila wanachama wanaombwa kumchangia chochote walichonacho. Kwa maelezo zaidi jinsi ya kutuma pesa wasiliana na Mwenyekiti Said Mchanjama. Ahsanteni. Katibu
Monday, 21 May 2012
ACCOUNT NUMBER
Asalaam Aleykum, Alhamdullillahi tumepata account, Islamic Bank of Britain wametukubalia kufungua account na wameshatuma account number pamoja na online banking account. Kuhusu Account number na maelezo zaidi ya jinsi ya kuweka ada ya kila mwezi mtayapata siku ya kikao ama wasilianeni na mweka hazina Fathiya Said Tel: 07878081832.. Ahsanteni.. Katibu
Friday, 18 May 2012
MKUTANO WELLINGBOROUGH
Asalaam Aleykum... Mkutano utafanyika tarehe 23/06/2012 na hii ndiyo address 5 Teal Lane, Wellingborough, NN8 4TT. Kwa maelezo zaidi ama ukipotea wasiliana na Mrs Mwanana Zuber Tel 07950515455/ 07950515450 Email mwanaana50@hotmail.co.uk. Ahsanteni na InshaAllah nawaombeni wanachama wote mfike, Katibu
KUHUSU SHADHILY BANK ACCOUNT
Naombeni msamaha kwa usumbufu uliojitokeza wa account number. Tulitegemea tutakuwa na account yetu ya chama haraka iwezekanavyo lakini tulipojaribu hatukufanikisha. Inshaalah tutajaribu Islamic Bank of Britain. Kwahiyo nitajaribu kumtumia kila mwanachama account number ya muda au ikiwezekana nije nayo kwenye kikao naomba maoni yenu? samahanini sana kwa usumbufu. Mweka hazina Fathiya Said Tel: 07878081832
BBQ
Wanachama wote tumekubaliana kufanya BBQ siku ya kikao, kwahiyo sote kwa pamoja tutakiwa kuchangia pesa za chakula kuanzia hivi sasa na mwisho wa kutoa mchango wa chakula ni tarehe 10 mwezi wa June. (Family £15 na single £10). Kuhusu jinsi ya kutuma hizo pesa kwenye account muone Ibrahim Salim ( Tel: 01908520736 au 07404489076) kwa maelezo zaidi na account number, Wabillah Tawufiq, Mwenyekiti Msaidizi Ibrahim Salim
Subscribe to:
Posts (Atom)